WELCOME !

THANK YOU FOR VISITING THIS SITE. I HAVE BEEN USING BOTH SWAHILI AND ENGLISH LANGUAGE TO EXPRESS ISSUES - I HAVE ATTACHED ENGLISH VERSION TO SOME OF THE SWAHILI NEWS/STORY AT THE END.

Tuesday 17 April 2018

TASKRABBIT YAKIRI KUDUKULIWA



KWA UFUPI: TaskRabbit imekua muhanga wa uhalifu mtandao – IKEA, Imethibitisha. Hii ni katika muendelezo wa Programu tumishi (Applications) na huduma zingine za kimtandao kuingiliwa na wahalifu mtandao ambapo taarifa za watu zimejikuta katika mikono isiyo salama.
---------------------------------
TaskRabbit iliyo anzishwa mwaka 2008 na Bi. Leah Busque iliyokua na madhumuni ya kutoa ajira zisizo rasmi kwa watu ambapo ilinunuliwa na IKEA mwaka 2017. Imekua ikitoa huduma zake kwa kujitegemea ndani ya mjumuiko wa makampuni ya nayo milikiwa na IKEA.

Program tumishi hiyo imekua ikitumiwa Zaidi na Raia wa Uingereza na maeneo mengine kujitafutia ajira zizizo rasmi kama kazi za ndani, kazi za bustani na nyinginezo ambapo wateja wa program tumishi hiyo na huduma za kimtandao zinazo shabiana na program tumishi hiyo imekua ikikusanya taarifa za watafuta ajira na wanao tafuta wakuwafanyia kazi hizo.

Mjadala wa wanausalama mtandao umeeleza taarifa binafsi nyingi za wateja zimekua zikikusanywa na sasa zimeingia mikononi mwa wahalifu mtandao. Prorgram tumishi pamoja na tovuti zimefungwa kwa muda kufuatia tukio hili.


Kamishna wa mawasiliano wa uingereza aamekiri kua na taarifa juu ya tukio hilo na ameeleza wanalifatilia kwa karibu. Aidha, TaskRabbit hadi sasa imekaidi kutoa ufafanuzi wa uhalisia wa tukio husika huku ikikadiriwa udukuzi umeathiri kwa kiasi kikubwa na huwenda umedumu kwa muda.

Kampuni imeeleza inafanya uchunguzi wa kina kufuatia tukio hilo huku ikewataka wateja wake kubadili maneno siri (Nywila) na kuahidi kutoa taarifa zaidi baada ya uchunguzi kukamilika juu ya athari Zaidi sanjari na kuwahakikishia wateja wake walioshindwa kufanya kazi zao kutokana na hitlafu zilizopelekea kufungwa kwa muda kwa huduma watapatiwa fidia.


NINI CHA KUJIFUNZA?

WAMILIKI WA PROGRAM TUMISHI: Kumekua na msisitizo mkubwa kwa wanaotoa huduma za mitandao ikiwa ni pamoja na program tumishi kutakiwa kuhaki wanajipanga kulinda taarifa za wateja wao kabla ya kuanza kutoa huduma.

Aidha, Kutokana na wimbi kubwa la wahalifu mtandao kuingiza tarikishi zisizo salama kwenye program tumishi bila ya wamiliki kua na ufahamu – Tumetoa muongozo mpya wa kuhakiki wamiliki wanalinda wateja/ watumiaji na endapo itatokea wahalifu mtandao wakadhuru wakuwajibishwa awe ni mmiliki.

Itakumbukwa tukio la Uber ambapo mamilioni ya taarifa za watumiaji wa program tumishi hiyo maarufu kwa kutafutia watu usafiri ilijikuta matatani baada ya kutoa mwanya wa wahalifu mtandao kuingiza tarikishi zisizo salama zilizo pelekea mamilioni ya Taarifa kuingia mikononi mwa wahalifu mtandao.

WATUMIAJI WA PROGRAM TUMISHI: Awali ya yote kila mtumiaji wa program tumishi yoyote anatakiwa kutambua anajukumu la kutambua faragha yake inalindwa vipi na program tumishi husika.

Kumekua na nahatua mbali mbali ambazo tumekua tukizichukua kuhaki taarifa binafsi za watu zinakua salama lakini pia ni jukumu la mtumiaji kufuata maelekezo tunayo yatoa.

Mfano:
-         Kabla ya kupakua na kuijumuisha program tumishi katika simu yako, mahitaji yanakuwepo? Na ulazima wakua nayo unakuwepo?
-         Unaifahamu vizuri progam tumishi uitumiayo? Hususan inachochukua kutoka kwako kabla ya kukupatia huduma?
-         Unatoa ruhusa wa taarifa chache pekee kuenda kwenye program tumishi au unaipatia taarifa nyingi zaidi zinazo hatarisha faragha yako?
-         Unatumia Nyila madhubuti na kibadilisha mara kwa mara kujilinda binafsi?

Pamoja na jitihada kubwa ambazo tumeendelea kuzichukua – Changamoto kubwa imekua watumiaji wamekua na uelewa mdogo wa namna ya kujilinda binafsi inayo pelekea matukio ya faragha za watu kuingia mashakani kutokana na kuendelea kukua kwa uhalifu mtandao maeneo mengi duniani.




No comments:

Post a Comment