WELCOME !

THANK YOU FOR VISITING THIS SITE. I HAVE BEEN USING BOTH SWAHILI AND ENGLISH LANGUAGE TO EXPRESS ISSUES - I HAVE ATTACHED ENGLISH VERSION TO SOME OF THE SWAHILI NEWS/STORY AT THE END.

Sunday 4 December 2016

MWANA USALAMA MTANDAO BORA WA MWAKA

Nikitoa Neno la Shukran
Pembeni Ni - Abner Abaga
(ICT Director - Wizara ya ICT,Kenya)
Mwishoni mwa mwezi wa kumina moja (Novemba) mwaka huu (2016) Jijini Nairobi Nchini Kenya, Nilibahatika kuibuka mshindi wa tunzo ya mwanausalama mtandao bora wa mwaka (Cybersecurity Expert of the Year) – Ikiwa ni kutambua mchango wangu mkubwa katika mataifa mbali mbali barani Afrika kuhusiana na swala zima la usalama mtandao.

Mchango wangu haujakomea Barani Afika, Nimekua pia nikitoa Mchango katika mataifa mengine mengi nje ya Bara la Afrika. Kutokana na Tunzo niliyopokea, Imeniongezea nguvu na hari mpya ya kutumikia fani yangu vizuri kwa manufaa ili kuhakiki situ tunapata Bara salama bali dunia salama kimtandao.

Kwa mujibu wa BBC kama inavyo someka “HAPA” – Imeelezea mchango wangu kua chachu ya kufanya mataifa mengi barani na nje ya bara kua salama. Aidha, kufuatia mahojiano yango na BBC nilipo ulizwa juu ya safari yangu Nchi Afrika kusini kuzungumzia zaidi Uchunguzi wa makosa mtandao mabapo tovuti kadhaa zimekua ziki ripoti Moja wapo ikiwa ni ya ITWeb kama inavyo someka “HAPA” nilieleza ya kua ifikemahali kila mmoja ajiulize atadhuriwa kimtandao lini na si kujiuliza kama anaweza kudhuriwa kimtandao.

Kurudi na Kikombe cha Tunzo nyumbani na mapokezi yake kwenye vyombo mbali mbali vya Habari vimeniongezea faraja zaidi – Niliendelea kusisitiza juu ya kuhakiki swala la usalama mtandao halibaki kua la kundi flani la watu, Pia kila mmoja ana dhamana ya kuhakiki anajilinda binafi dhidi ya wahalifu mtandao.


Aidha, Makampuni na Taasisis mbali mbali lazima ziwe na vitengo rasmi vitakavyo shughulikia maswala ya usalama mtandao pamoja na Taifa kwa ujumla kufunga mikanda zaidi katika kukabiliana na wimbi kumbwa la uhalifu mtandao unao kua kwa kasi.


Wahalifu mtandao hawalali, na kila siku wanakuja na mbinu mpya za kufanya uhalifu mtandao – Itashangaza kama wadhibiti (Wanausalama mtandao) watashindwa kuendana na kasi ya namna mpya za uhalifu mtandao. Ili kufikia hili lazima kila siku kuwe makini na maelekezo tunayo yawasilisha kutoka maeneo yote duniani juu ya hali ya usalama mtandao sanjari na gunduzi mpya za uhalifu mtandao.

Mfano, Kwa sasa Ma benki na Makampuni ya simu ni moja ya maeneo yanayo windwa sana na wahalifu mtandao na hadi sasa wamefanikiwa kudhuru mataifa makubwa kama Urusi, Ujerumani , Uingereza na kadhalika. Hivyo Mataifa mengine lazima yajue kinachoendelea na kuhakiki wana jipanga kudhibiti athari zozote na kama athari zitazikumba basi kuwe na timu sahihi yenye watu sahihi watakao weza kutatua tatizo mara moja.


Nilipo hudhuria uzinduzi wa ripoti ya hali ya usalama mtandao kwa baadhi ya Nchi za Afrika iliyofanyika Serena jijini Dar-es-salaam Nililiona changa moto kubwa ya kuto ripotiwa matukio ya kihalifu mtandao imeendelea kusababisha twakwimu sahihi kutopatikana na kufanya utambuzi wa wapi kwenye tatizo zaidi kuto gundulika – Kwenye hili lazima tubadilike.

Kwa mujibu wa Ripoti wasilishwa na wazungumzaji mbali mbali nikiwepo,  asilimia 91 (91%) ya matukio ya kihalifu mtandao hayaripotiwi, Kuna mahitaji ya wana usalama mtandao Elfu thelathini (30,000) zaidi Nchini, hasara ya zaidi ya dola milioni 85 ($85M) imesababishwa na uhalifu mtandao kwa mwaka huu pekee, huku Eng. Petter wa UCSAF – akieleza ya kua zaidi ya matukio elfu moja mia nane (18000) yalijitokeza mwaka jana pekee ndani ya Tanzania.

Takwimu hizi si nzuri sana kwa Taifa – Na tunawajibu wa kufanyia kazi ziweze kupata suluhu. Hivyo tuanze na utayari wa kutambua uhalifu mtandao ni janga, kisha tupange timu mpya sahihi ya kukabiliana na janga hili na hakika mambo mengine yote yatafata kwa urahisi zaidi. Aidha nilitoa wito kwenye mkutano huo juu ya mambo kadhaa yakiwemo kuhakiki tunakua na familia rasmi ya wana usalama mtandao kama si ya wana TEHAMA kwa ujumla ili kuweza kurahisisha kubadilishana taarifa na uzoefu. Pia kutambua michango mizuri ya watu ni jambo muhimu sana.


 Kua katika fani ya usalama mtandao na kuhakiki unatumikia fani hii kwa manufa ili mataifa mbali mbali yabaki salama na sio kuharibu ni jambo ambalo wengi bado limewawia vigumu. Hii ndio inapelekea kua na makundi makubwa matatu ya wanaofahamu maswala ya usalama mtandao ambayo ni wale wanaojua na wakadhuru wangine (Whalifu mtandao) , Wanao jua na wakasaidia watu (Wanausalama mtandao), Na walio katika kundi la kati (Mchana – Wanausalama mtandao na usiku – Wahalifu mtandao).


Kundi la tatu ni kundi ambalo kupitia mikakati madhubuti linaweza likachukuliwa na wanausalama mtandao na kutokua na mikakati madhubuti ni rahisi kutekwa na wahalifu mtandao kitu ambacho kitaongeza wimbi la wahalifu mtandao na kusababisha ukuaji wa kasi wa uhalifu mtandao.


No comments:

Post a Comment