WELCOME !

THANK YOU FOR VISITING THIS SITE. I HAVE BEEN USING BOTH SWAHILI AND ENGLISH LANGUAGE TO EXPRESS ISSUES - I HAVE ATTACHED ENGLISH VERSION TO SOME OF THE SWAHILI NEWS/STORY AT THE END.

Saturday 30 April 2016

WIZI MTANDAO KWENYE TAASISI ZA FEDHA BADO NI CHANGAMOTO

Teknolojia imeendelea kurahisisha maisha na kwa sasa kumekua na ukuaji wa matumizi ya simu za viganjani kufanya miamala ya fedha maeneo mengi ya bara la Afrika. Kufuatia ongezeko kubwa la watumiaji wa simu, mabenki na kampuni za simu zimeendelea kuhakiki simu zinatumika kufanya miamala ya kifedha.

Kwa mujibu wa ripoti ya mwaka jana (2015) ya GSMA State of the industry, huduma za kifedha kupitia simu kwa sasa zinapatikana katika nchi 93 duniani ikiwa na jumla ya huduma 271 kwa ujumla wake, kwa wastani watoa huduma za kifedha kupitia simu wana safirisha kiasi cha dola milioni 33 kwa siku. Takwimu hizi  zinategemewa kuendelea kukua.

Aidha, Mwaka jana (2015), European investment bank ilianisha Afrika kuongoza duniani kwa matumizi ya Simu za viganjani kufanya miamala yakifedha. Kwa Upande wa Nchi ya Kenya, asilimia 62 (62%) ya watu wake wamekua wakitumia simu za viganjani kufanya miamala ya kifedha.

-------------------------------------
NEWS UPDATE: Some of the contributing factors in the US $80 million theft from the Bangladesh central bank included the use of inexpensive, second-hand routers and the lack of a firewall. In addition, an investigation conducted by BAE Systems suggests the attackers tricked the SWIFT financial software with custom malware.
--------------------------------------

Imefika wakati, Tunaweza kulipia huduma mbali mbali, kuhamisha fedha, kununua bidhaa, na mambo mengine kadhaa kupitia simu zetu za viganjani. Urahisi huu katika maisha pia umeambatana na ukuaji wa wahalifu mtandao wanaoendelea kwa kasi kuja na njia tofauti tofauti kufanikisha wizi wa fedha zinazo patikana au kuhamishwa kupitia simu zetu za mikononi.


Kwa mujibu wa ripoti ya 2014 ya ACFE, The Nationals on occupational Fraud and abuse inaeleza kupitia kesi 1,483, dola bilioni 3 zimepotea kutokana na wizi mtandao. Aidha, Kila mwaka Nchi ya Kenya pekee inapoteza kiasi cha Shilingi bilioni 5 za kenya (sawa na Dola milioni 50) huku ikitabiriwa kiasi hicho kinaendelea kuongezeka.
Mabenki yameendelea kutumia teknolojia ya neon la siri la mara moja (One time Password – OTP) kama njia kulinda fedha za wateja wake ambapo teknolojia hii tayari imekuwepo kwa muda mrefu sasa – Imepitwa na wakati.

Itakumbukwa mwaka 2012, Australia ilionya mabenki kutotegemea mfumo wa message kutoa taarifa miamala kwani sio salama sana na kuzitaka zibuni njia mpya ambayo ni salama zaidi.

Hili linathibitishwa na wataalam mtandao kutokana na ongezeko kubwa la uhalifu aina ya Man in the middle attack ambapo mhalifu anakaa baina ya watu wa wili wanaofanya mawasiliano hasa miamala ya kibiashara na kufanikiwa kusoma na kuchukua taarifa zinazo safirishwa na baadae kuzitumia taarifa hizo kuiba pesa kwenye mitandao au kupata taarifa za watu.

Mbali na hilo, wengi wame endelea kuathiriwa na uhalifu wa Phishing attack ambapo zinatengenezwa programu tumishi feki, kutumiwa barua pepe zenye mlengo wa kukusanya taarifa na mambo mfano wa hayo ya kidanganyifu ili kuweza kufanikisha wizi wa taarifa pamoja na fedha.

Tukijadili changamoto mbali mbai nchini Kenya zinazokabili taasisi za kifedha hasa zinazotumia huduma ya fedha kupitia simu za viganjani (Mobile banking), tuliweza kuangazia mapungufu mbali mbali ambayo bado tunayo katika bara na hasa ukanda wa Afrika mashariki ambapo huduma za kifedha kwa njia ya simu ndio zimeshika kasi.

Binafsi niliwasilisha mada ya aina mbali mbali za wizi mtandao hadi sasa na namna ya kukabiliana nazo, mahali tulipofikia hadi sasa kupitia matukio kadhaa makubwa na mbino zilizoweza kutumika kama ambavyo tumekua tukijadili katika vikao mbali mbali na mwisho nika zungumzia swala zima la kukabiliana na wahalifu wa ndani kitaalam tunawaita insider threats ambao wameendelea kuwa tishio kubwa kwa taasisis za kifedha.

Kwan chi ya Kenya mbali na uhalifu huu wa wizi kupitia mitandao kuwa juu zaidi, Tanzania nayo imeonekana kua na matukio mengi ya aina hii ambapo kwa ujumla tuliangazia macho kwa ukaribu ili kuweza kutafuta suluhu kupitia mijadala tuliyo kua nayo kwa siku tatu mfululizo.

Muhimu ninayopenda kuasa taasisi za kifedha ni pamoja na :-

Kujenga tabia ya kutoa elimu kwa uma ya uelewa juu wa namna ya kulinda pesa zao hasa wafanyapo miamala kupitia mitandao ya simu au kupitia tovuti. Hili litasaidi kupunguza idadi ya wanaojikuta kuingia kwenye matatizo ya kihalifu mtanda (Kupoteza pesa zao) kwasababu tu ya kukosa uelewa.

Kuhakiki wanaoshughulikia moja kwa moja udhibiti wa wizi wa fedha katika taasisis za fedha wanapatiwa ujuzi wa kujua mbinu mbali mbali wahalifu mtandao wanatumia kufanikisha wizi wa fedha na namna ya kukabiliana nao. Uchunguzi niliofanya nimegundua kiasi ni kidogo sana cha wadhibiti hawa wanao jua matukio kadhaa ambayo yameendelea kutokea ya wizi wa fedha na namna yalivyo tokea sanjari na hatua zilizo chukuliwa kukabiliana nayo. Hii inadhihirisha kuna tatizo kubwa la ufatiliaji ambapo lazima liboreshwe kwa kupatiwa elimu na kuhimizwa kua natabia ya kufatili matukio.

Kuna njia mbali mbali ambazo kwa ujumla wataalam mtandao wamekubaliana kimsingi zifatwe ili kuweza kuzuia, na kama matukio yamejitokeza- basi namna ya kukabiliana nayo ambazo ni nyingi kuzianisha zote kupitia andiko hili, lakini lazima wahusika wajue na waingize katika vitendo.

Matumizi ya teknolojia mpya zinazo weza kusaidia kupunguza wizi huu ikiwa ni pamoja na kutotumika kwa Windows XP katika mashie zetu za kutolea fedha (ATM)  pia ni muhimu kuangaziwa macho kwani kimsingi matukio kadhaa ya hivi karibuni yamebainika yamejiri kutokana na matumizi ya vifaa chakavu na vilivyopitwa na wakati  vya ulinzi katika taasisis za kifedha pamoja na kuwa na umakini mdogo katika vifaa vinavyo saidia ulinzi ndani ya taasisis za kifedha.

Nitoe wito kwa taasisi za kifedha kuhakiki ushauri wa kitaalam unaotolewa unafanyiwa kazi ili kuweza kulinda fedha za wateja wao. Nchi ya Kenya imefanikiwa kuweka mifumo mbali mbali kwenye taasisi za kifedha inayo mpa fursa mtumiaji kujua kupitia jumbe pesa zinapotoka kwenye akauti zao ambapo huduma hii ni kwa mabenki takriban yote.

Aidha, wamekua na taratibu zinazfatwa na taasisi za kifedha za kuhakiki fedha za wateja wa taasisi za kifeda zinabakishwa salama na kimsingi pale taasisi inapo kiuka chombo cha serikali kinachodhibiti kinachukua hatua stahiki.


PICHA: Picha ya Pamoja ya baadhi ya washiriki wa kikao maalim kilicho kamilika Nchini Kenya kilichokua na mleno wa kuangazia uhalifu mtandao unaoendelea kukua kwa kasi wa wizi wa fedha kimtandao katika taasisi za fedha hasa zinazotumia huduma kupitia simu za viganjani.


Kwa upande mwingine, nikiwa Nchini Kenya – Nilipata fursa ya kubadilishana mawazo na watu kadhaa ikiwamo pamoja na Waziri wa Nchi hiyo wa mambo ya ndani, Mh. Joseph Nkaissery ambapo pia nilimpongeza kwa kazi yake nzuri anayo ifanyia taifa lake.

No comments:

Post a Comment