WELCOME !

THANK YOU FOR VISITING THIS SITE. I HAVE BEEN USING BOTH SWAHILI AND ENGLISH LANGUAGE TO EXPRESS ISSUES - I HAVE ATTACHED ENGLISH VERSION TO SOME OF THE SWAHILI NEWS/STORY AT THE END.

Thursday 30 April 2015

KATIKA KUELEKEA KUAPATA TAIFA SALAMA KIMTANDAO

Taarifa “INAYOSOMEKA HAPA” ilitolea ufafanuzi wa Nchi ya India inavyo pambana ili kuweza kufikia malengo katika kuboresha usalama mitandao hasa katika wizi unaofanywa kupitia ATM. Na baada ya kupata kutolea ufafanuzi muswada wa sharia mtandao, taarifa “INAYOSOMEKA HAPA”  Ilifafanua yamuhimu kuzingatia ili sheria hiyo iweze kupelekea kufikiwa kwa malengo kusudiwa ya kupata Tanzania salama kimtandao na kupunguza wimbi la makosa mtandao nchini.

Baada ya hayo nilipata kuhudhuria mikutano kadhaa katika nchi mbali mbali ambapo nilifanikiwa situ kuwasilisha mada kwa wataalam wengine wa maswala ya usalama mitandao bali pia kujifunza mengi kutoka kwao katika maswala mbali mbali ya msingi ya kufanyiwa kazi ili kuweza kuboresha usalama mitandao situ katika ngazi ya kitaifa bali na kibara pamoja na  Dunia kwa ujumla.

Makubwa matatu ambayo nimeona niyazungumzie leo ni pamoja na kuhakiki kuna njia madhubuti na zenye mpango stahiki za kukuza ulewa kwa watumiaji mitandao jinsi ya kujilinda na kulinda wengine watumiapo mitandao, Kuhakikisha Taifa linakua na mikakati endelevu ya kutengeneza na kuongeza uwezo wataalam wa maswala ya usalama mitandao pamoja na kupatikana na ufumbuzi wa kudumu wa kukabiliana na wimbi la wizi wa fedha kupitia mashine za ATM.

Nilipokua Nchi KENYA nilipata kuwasilisha mada mbali mbali pamoja na kuwa na mazungumzo na washiriki mbali mbali nchini humo kuhusiana na nini kinacho kwamisha kufikiwa kwa malengo ya program zinazofanywa zenye malengo ya kukuza uelewa wa matumizi salama ya kimtandao.

Katika hili – Nimeona tatizo kubwa ni kuwa na udhaifu mkubwa katika maandalizi na ufahamu wa namna ya kuwasilisha program zenye malengo ya kukuza uelewa wa matumizi salama wa mitandao. Ili kujua hili kuna taarifa “INAYOSOMEKA HAPA”  itakayoweza kutoa yakuzingatia wakati wa kuandaa program za kukuza uelewa wa matumizi salama ya mitandao “Awareness program”.


Nchini ZIMBABWE, Kubwa nililoliona nila jitihada za kuhakiki Bara la Africa linakua na tabia ya kukuza wataalam wake ili kuweza kukabiliana na changamoto mbali mbali za kiteknolojia huku suluhu ya wizi wa fedha kupitia ATM ni muhimu kuangazikwa kwani wizi huo umekua ukisababisha kuyumba sana kwa uchumi. Hili lilionekana pia katika mkutano mwingine wa Kenya kama taarifa “INAYOSOMEKA HAPA”  inavyo fafanua. 

1 comment:

  1. brother nimekuandikia katika page yako ya Facebook
    Naomba unijibu ni muhimu sana.
    Ahsante.

    ReplyDelete