WELCOME !

THANK YOU FOR VISITING THIS SITE. I HAVE BEEN USING BOTH SWAHILI AND ENGLISH LANGUAGE TO EXPRESS ISSUES - I HAVE ATTACHED ENGLISH VERSION TO SOME OF THE SWAHILI NEWS/STORY AT THE END.

Thursday 21 August 2014

UCHAMBUZI: NJIA ZA KUPAMBANA NA UHALIFU MTANDAO

Suala la hivi karibuni la nchini Israel la kiusalama mitandao linaloweza kusomeka "HAPA", Polisi wanchi ya Botswana kuonyesha wasi wasi wao juu ya maswala ya usalama mtandao kama inavyoweza kusomeka "HAPA" pamoja na matukio mengine kadhaa ya uhalifu mitandao ambayo yamekua yakigonga vichwa vya habari hivi sasa yameibua swali, je kuna uwezekano mapambano dhidi ya uhalifu kufikiwa malengo kwa kupunguzwa walau kwa kiasi Fulani?

Jibu ni kwamba hivi sasa uhalifu mtandao umeendelea kukua huku pakitumika njia za kisasa na hatarishi zinazo onekana kua tishio katika mifumo ya mitaandao katika nchi nyingi duniani. Ingawa pia  wataalam wa maswala ya usalama mitandao wameendelea kujipanga na kuangalia kila namna ya kuweza kukabiliana na uhalifu mtandao katika ngazi ya kidunia.

Kubwa lililo jiri hivi karibuni kumeendelea kutafutwa mbinu za kuhakiki uhalifu mitandao unapata kudhibitiwa huku baadhi ya makampuni nanchi mbali mbali kuchukua hatua stahiki nikitolea mfano "FACEBOOK" na tukio la "UJERUMANI" ikiwa ni mifano miwili kwa uchache.

Lakini pia azimio la hivi karibuni lililokua limebeba mambo ma tano (5) limeendelea kufanyiwa kazi katika mataifa mbali mbali ambapo yatatoa fursa ya kuweza kupunguza na kuzuia uhalifu mtandao katika maeneo husika. Mambo hayo ni pamoja na kukuza uelewa wa maswala ya usalama mitandao kwa wananchi ( Cyber security awareness programs), Kuwa na Sheria za usalama mitandao ( Cyber laws) , Kuweza kukuza uwezo wa wataalam wa ndani katika mataifa mabali mbali ( Capacity building).


Mengine ni pamoja na Kuwa na uwazi wa takwimu za kiuhalifu mtandao ( Cybercrime statistics) pamoja na kupatikana kwa makubaliano ya pamoja ya nchi katika mabara ili kuweza kuunganisha nguvu ya pamoja kwenye mapambano dhidi ya uhalifu mtandao ( Cybersecurity framework).

Kwenye andiko hili nitatolea ufafanuzi juu ya mambo hayo matano na jinsi gani yanavyoweza kusaidia mapambano dhidi ya uhalifu mtandao huku nikitolea mifano kadhaa.

CYBERSECURITY AWARENESS PROGRAMS: Inaaminika ni vizuri kujikinga na tatizo kuliko kungoja litokee kisha litaftiwe tiba. Na pia inaaminika tatizo linaweza kuzuiwa kuanzia katika ngazi ya mtu moja mmoja. Kila Mmoja anapoweza kujiweka salama mtandaoni atasababisha uhalifu kupungua na kutoa urahisi kwa wana usalama mitandao kuweza kupambana na uhalifu huo.

Hivyo jukumu la kila mtu kujijengea muda wa kutaka kujua namna za kuweza kukaa salama kimtandao ni muhimu sana. Tasnia ya habari michezo na maigizo kupitia vipeperushi, Sinema , maandiko mengine yanaweza kutumika kuweza kukuza uelewa kwa wananchi kujua namna ya kua salama na hatimae kujenga uelewa wa kujikinga na uhalifu mtandao kuanzia katika ngazi ya mtu mmoja mmoja.

CYBER LAWS: Hizi ni sharia mitandao. Ni vigumu sana kwa mahakama kuweza kutoa hukumu stahiki kwa wale wote wanaoweza kukamatwa kwa maswala ya uhalifu mitandao ikiwa hapata kuwa na sheriashariai inayo kidhi mahitaji ya maswala ya ulinzi mitandao.

Hili limekua likionekana kua kikwazo kikubwa nanchi nyingi zimeendelea kuchukua hatua za kuboreshwa sharia mtandao zilizo kuwepo ili kwenda na wakati (Mfano: "UINGEREZA") pamoja nanchi nyingine kuazisha sharia hizo ili kuweza kusaidia kutoa hukumu kwa wahalifu mtandao (Mfano: "TANZANIA")

CAPACITY BUILDING: Hili la kukuza uwezo wa ndani kwa wataalam wa maswala ya usalama mitandao ili kuweza kupata watakao kua na ujuzi sahihi wa uhalifu mtandao na namna ya kuppambana nao pia imeendelea kua muhimu sana. Nilipata kuhojiwa na chombo kimoja cha ughaibuni na baadae kuwekwa hili vizuri kama linavyo someka "HAPA"ambapo msisitizo juu ya kila nchi kuweza kujenga miundo mbinu ya kuweza kukuza vipaji vya wataalam wake wa ndani wa maswala ya usalama mitandao ni muhimu sana ukizingatia uhaba mkubwa ulioko wa wataalam wa maswala ya usalama mitandao kote duniani.

Nchi nyingi kwa sasa zimeendelea kulichukulia hili uzito na tayari limeendelea kufanyiwa kazi ikiwa ni pamoja na Marekani, Visiwa Vya Solomoni, Uingereza na Afrika Kusini kutaja nchi kwa uchache. Uzuri kwa Tanzania Pia Hili huwenda likawa na sura nzuri hivi karibuni ambapo itakua ni fursa kwa watanzania kulichangamkia  ili kuweza kuendana na hali ya ukuwaji wa teknolojia hivi sasa.

CYBERCRIMES STATISTICS: Hili lakuwa na takwimu za uhalifu mitandao zinazowekwa wazi limekua likisisitizwa liweze kufanyiwa kazi na kubainishwa kupitia ripoti za mwaka za nchi moja moja ambazo baadae zinaweza kujumuishwa kwenye ripoti za mwaka za kimataifa ambazo zitatoa fursa ya kutambua maeneo hatarishi ili kuweza kukabiliwa kwa haraka na kupatiwa nguvu ya muunganiko.

Aidha, Kupitia Tovuti maalum zinazojihusisha na mapambano dhidi ya uhalifu mtandao au za serikali za nchi moja moja pia zimeonekana kuwa na nafasi katika hili huku nchi ya "SIRILANKA" kuonyesha mfano kwenye hili pamoja na Nchi nyingine kadhaa.

CYBERSECURITY FRAMEWORK: Hili limekua ni la muhim sana chini ya mwamvuli wa umoja ni nguvu na utengano ni udahifu. Mapambano ya uhalifu mtandao ni magumu sana endapo nchi moja moja itachukua dhamana binafsi bila kushirikiana na nyingine kwa ukaribu kwa kuunganisha nguvu.

Hili linatokana na uhalisia wa uhalifu mtandao mbali na kua na uharibifu mkubwa sana katika mataifa mbali mbali bali pia hauna mipaka. Hapa naamanisha mhalifu mtandao hana ulazima wakua katika eneo la tukio au kua katika nchi anayo tegemea kuifanyia uhalifu, Maana yake Mhalifu aliye nchi moja anaweza kuleta madhara makubwa sana katika nchi nyingi pasi nayeye kuwai kufika katika nchi hiyo.


Kwa kuliona hili Nchi za Umoja Wa Ulaya (EU) Walifanikiwwa kuja na makubaliano yao yapamoja yaliyo unganisha nguvu nchi zote wanachama pamoja na kuwa na kituo mama kinachoshughulikia maswala yao ya usalama mtandao na takwimu zinaonyesha wamefanikiwa kwa kiasi kikubwa katika mapambano baada ya kuanzishwa kwa umoja huo wa kushughulikia maswala ya usalama mitandao ambapo walipata kusifiwa kufuatia hatua yao hiyo kupitia taarifa inayosomeka "HAPA"

No comments:

Post a Comment