WELCOME !

THANK YOU FOR VISITING THIS SITE. I HAVE BEEN USING BOTH SWAHILI AND ENGLISH LANGUAGE TO EXPRESS ISSUES - I HAVE ATTACHED ENGLISH VERSION TO SOME OF THE SWAHILI NEWS/STORY AT THE END.

Friday 6 June 2014

WAHALIFU MTANDAO WAITIKISA KOLOMBIA

Polisi Wa  kuzuia uhalifu Mtandao.
Wakala unaofuatilia matumizi ya mitandao duniani (IAB) umebaini watumiaji wa intaneti nchini Kolombia wamekua ni asilimia 70 ya wakazi milioni 47 wa nchi hiyo huku ikibainishwa ya kuwa nchi hiyo ukuaji wa uhalifu mtandao umeendelea kukua kwa zaidi.

Mwaka 2011 Kolombia ilikua Nchi ya kwanza kuanzisha sera ya usalama mitandao katika ukanda wan chi za latini amerika kupitia baraza la taifa la nchini humo linaloshughulikia maswala ya sera za uchumi na kijamii (COMPES).

Kupitia Sera hiyo, Paliundwa kikundi kinachoshughulikia maswala ya mitandao kilicho unganishwa moja kwa moja na wizara ya ulinzi pamoja na polisi wa nchini humo kupitia kitengo kinachojiusisha na maswala ya ulinzi mtandao.


Pamoja Na jitada zote hizo bado nchi hiyo imeendelea kukumbwa na mamia ya uhalifu mtandao unaofanywa dhidi ya raia wake na serikali ya nchi hiyo na ndipo palipo anzishwa misheni inayotoa misaada ya kiufundi ya usalama mitandao jijini Bogota nchini humo.


Kolombia waliunganisha nguvu na wataalam kutoka nchi nyingine  kuanzia tarehe 31 ya mwezi machi hadi tarehe 4 ya mwezi aprili mwaka huu (2014) ili kupitia na kuchambua  hali ya usalama mitandao ya nchi yake na kutoa mapendekezo stahiki.

Bwana Belisario Contreras kutokea  (CICTE) alieleza ushauri na mapendekez yaliyo tolewa yataingizwa katika vitendo ili kukabiliana na asakata la uhalifu mtandao nchini humo.

Aidha, Erwin Doutzauer strampfer kutokea chuo kikuu cha Oxford alipokua akichangia hali ya uhalifu mtandao amenukuliwa akisema kutokana na uhaba mkubwa wa wataalam wa maswala ya ulinzi mtandao shabaya ni kuendelea kukuza nguvu watu na kusisitiza changamoto kubwa iliyoko sasa ni kuingiza mafunzo ya usalama mitandao kuanzia ngazi ya chini mashuleni ili kuwezesha vijana wadogo kujua jinsi ya kujilinda mitandaoni ambapo ameeleza kumekua na kesi za watoto kujiua kutokana na kile alicho kisema kama “Cyberbulling”.

Ufafanuzi wa hili kwa lugha ya kingereza unasomeka "HAPA" na taarifa ya awali ya kingereza  iliyo ainisha juhudi za nchi hiyo dhidi ya mapambano ya uhalifu mtandao pia inapatikana "HAPA" .

No comments:

Post a Comment