WELCOME !

THANK YOU FOR VISITING THIS SITE. I HAVE BEEN USING BOTH SWAHILI AND ENGLISH LANGUAGE TO EXPRESS ISSUES - I HAVE ATTACHED ENGLISH VERSION TO SOME OF THE SWAHILI NEWS/STORY AT THE END.

Sunday 1 June 2014

MAPAMBANO YA UHALIFU MTANDAO

Mbali na midahalo, hatua mbali mbali za kukabiliana na uhalifu huu wa kimtandao kwa sasa kumekuja na kasi ya kukuza nguvu watu ili kuongeza nguvu ya kukabiliana na uhalifu huu wa mitandao kwenye taarifa ya "NSA-YA MAREKANI"  imeweza kubainisha jinsi taifa hilo linavyo ongeza mafunzo kwa vijana wapya na kuanzishwa program maalum katika vyuo ambapo gharama za mafunzo hayo kwa vijana zinakua ni za serikali.

Hili pia limeonekana kwa nchi ya Afrika ya kusini kupitia mpango wa mafunzo ya mwezi mmoja ya jinsi ya kukabiliana na uhalifu mtandao ambapo yaliyodhaminiwa na kupewa jina la kumbukumbu ya Mandela.

Elimu imekuwa ikisambazwa kwa jamii kwa njia ya mbali mbali ikiwa ni kukuza uelewa wa hali ya uhali huu mpya wa kimtandao ambao unaaminika kuwa ni tishio hivi sasa wenye uwezo wakuleta madhara makubwa na hauna watu wakutosha kuweza kukabiliana nao.

Hili Limedhihirika kwenye hatua zinazo chukuliwa na "HOLLYWOOD" kutoa elimu kwa jamii kupitia tamthilia na filamu mbali mbali, pia baadhi ya waimbaji kuingiza maswala ya ulinzi mtandao kwenye nyimbo zao.



WITO

Imefika wakati sasa kwa Tanzania nayo kuangaza macho kwenye swala hili la uhalifu mtandao kwa kuhakiki raia wake wanapata elimu ya kutambua makosa mtandao na namna ya kujenga hatua za awali kukabiliana nayo katika ngazi ya mtu binafsi. Hili linaweza kufikiwa iwapo tasnia ya habari na sanaa itashirikishwa kwenye hili.

Kuandaa nguvu watu kwa kuweka mafunzo nchini ili kuwezesha vijana wengi nchi kujifunza ujuzi huu pasi na kusafiri kwenda mbali kutafuta elimu ya maswala ya ulinzi mtandao.

Mahitajio ya wataalam wa maswala ya ulinzi mtandao yanazungumziwa kukua kwa kasi na hili lilionekana kwenye taari niliyoiandikia  "CYBERSECURITY DEMAND" kwa kuliangalia hili uweo wa wataalam hauna budi kujengwa kuanzia ngazi ya kitaifa ili kujengea utayari wa kukabiliana na uhali mtandao pasi kuhitaji msaada kutoka kwa wataalam w a nje pale tatizo linapo kuwa nchini – Tujipange na tujenge tabia ya kuzuia tatizo pasi kusubiri litokee na kuwa kubwa.

Kuwa na sharia zinazoenda na wakati katika maswala haya ya uhalifu mtandao, Nchi nyingi hivi sasa zimeanza tena kupitia upya sharia zake za uhalifu mtandao na kuziboresha kutokana na mabadiliko makubwa katika ukuaji wa teknolojia. Mfano 3D printa ambazo zimeonekana kuleta athari kubwa sana kwenye maswala ya usalama mtandao yamepelekea mataifa kadhaa kupitia upya sharia zake.

Hili pia limeonekana kwa nchi kadhaa ambapo hazikua na sharia rasmi kuingiza maswala haya ya uhalifu mtandao ikiwa ni pamoja na "TANZANIA" ingawa kwenye hili Tanzania bado ina safari kwa kupitia na kuborehsa kila inapo paswa sharia hizi za mitandao kwani hazifanani kabisa na sharia za kawaida kutokana na mabadiliko ya teknolojia kila kukicha ambayo yanaadhiri moja kwa moja maswala ya uhalifu mtandao.

Kujenga utamaduni wa kufatilia maangalizo mbali mbali ya kiusalama mtandao, Inasikitisha sana kuona sit u Tanzania bali nchi nyingi kuwa karibu sana kufatilia maswala tofauti tofauti mbayo huwenda si yamsingi kabisa na kutokua na ufatiliaji wa maswala ya muhimu ambayo yanaweza kuathiri moja kwa moja Maisha yetu ya kimtandao.

Ni ukweli watumiaji wa mitandao nchini wamekua kwa kasi nani vizuri kila mmoja wetu kujenga tabia ya kupitia pale taarifa za maswala ya uhalifu mtandao yanapokua yakijadiliwa ili kupata uelewa wa kukabiliana nayo katika ngazi ya mtu binafi.


Hii pia iwawezeshe waandishi wa habari kujitahidi kufatilia na kuhabarisha jamii juu ya maswala haya ya ulinzi mtandao.

No comments:

Post a Comment